Hakimiliki ya picha: Soka La Bongo
TETESI za usajili zinadai kuwa Feisal Salum ‘Fei Toto’ amemalizana na Yanga SC, lakini kiungo huyo wa Azam FC ameibuka na kufunguka wazi kuhusu hatma yake kuelekea msimu ujao wa mashindano.
Fei Toto amesema kwa sasa bado ni mchezaji halali wa Azam FC, akiwa na mkataba wa mwaka mmoja zaidi, hana mamlaka ya kuzungumzia
mipango ya klabu nyingine yoyote.
“Siwezi kuzungumzia suala la Yanga, wala sifahamu kama kweli wameleta ofa au la, kwa sababu bado nina mkataba wa mwaka mmoja na Azam FC. Mimi ni mchezaji wao hadi hapo nitakapomaliza mkataba wangu,” amesema kiungo huyo.
Kauli hiyo ya Fei Toto imekuja kufuatia taarifa zilizozagaa kwamba tayari amefikia makubaliano ya kurejea Yanga SC, klabu aliyoitumikia kabla ya kujiunga na Azam FC.
Inadaiwa kuwa viongozi wa Yanga wamekuwa kwenye mazungumzo na wenzao wa Azam FC kwa lengo la kumrejesha kiungo huyo katika kikosi chao, wakiamini anaweza kuimarisha safu ya kiungo msimu ujao.
Fei Toto alijiunga na Azam FC akitokea Yanga SC msimu wa 2023/24, kwa mkataba wa miaka mitatu. Uhamisho wake ulihusisha matarajio makubwa ya kuongeza ubora katika eneo la kiungo wa ulinzi ndani ya kikosi cha Azam.
Kwa sasa, mashabiki wa soka wanasubiri kwa hamu kuona iwapo tetesi hizo zitageuka kuwa kweli au la, huku suala la uhamisho wake likibaki mikononi mwa klabu husika na uongozi wake binafsi.
Jisajili na Betway, burudika na kila tukio na amsha amsha ukibashiri kwenye ligi za mpira wa miguu kama;
Ligi Kuu ya Uingereza, La Liga, Ligi ya Mabingwa Ulaya na mengi zaidi.
Kwa habari zote za michezo, taarifa za kubashiri na promosheni tufuatilie
Betway kwenye kurasa zetu za
Facebook,
Twitter,
Instagram na
Youtube. Pakua App ya Betway.